Monday 18 November 2019

MATUMIZI BORA YA MAJI KATIKA KILIMO CHA MPUNGA NO. 2

Utangulizi: Karibuni tena wanazinduka na kilimo na wapenzi wafuatiliaji wa makala bora za kuhusu maswala ya kilimo (ZINDUKA NA KILIMO BLOG) ambayo inatoa fursa ya kuelimika na kuuliza maswali mbalimbali kuhusu maswala ya kilimo ikiwa ni hatua muhimu za kukabiliana na changamoto za kilimo tunazokumbana nazo siku kwa siku kama wakulima.

LEO: ni muendelezo wa somo la matumizi bora ya maji katika zao la mpunga.

Tumejifunza faida za matumizi ya maji katika zao la mpunga na zifuatazo ni muendelezo wa baadhi:-

  • Maji yakitumika kwa kidogo na kwa usahihi husaidia uongezwaji na ufunguliwaji wa vitivo na mashamba mapya ya mpunga na kuendelea kukuza vipato vya wananchi katika jamii husika.
  • Matumizi bora ya maji hupunguza gharama za uendeshaji na kuleta faida kubwa kwa mkulima hii ni kutokana na kupunguza idadi za uwekaji maji shambani pamoja na kupunguza bili za matumizi ya maji kwa baadhi ya skimu za mpunga hapa Tanzania (Water Right)

Hii picha ni mfano wa shamba linalofuata kanuni za matumizi bora ya maji
lipo katika skimu ya moshi 
MS 7-2 Block, Plot no 511










  • Sambamba na matumizi bora ya maji lakini pia kuna aina za mbegu za mpunga za muda mfupi na zinazo stahimili ukame na magonjwa pamoja na mavuno Mengi.
Baahdi ya aina hizo ni NERICA (NEW RICE FOR AFRICA) ambayo inaharufu nzuri, mazao mengi na inastahimili ukame, pia TXD 306 (Saro 5) ni aina ya mpunga inayofanya vizuri katika swala la mavuno mengi.

NB kipindi kijacho tutajifunza kwa undani kuhusu aina hizi mbili za mpunga na jinsi ya upatikanaji wakekwa watakao hitaji mbegu za mpunga.


Msisite kuuliza maswali kupitia blog na kupiga simu kwa ushauri na msaada kuhusu maswala ya kilimo na kuhitaji mbegu bora za mpunga
KIBAYA JASTINI SIMON, 
Mtariti wa mpunga, JIRCAS.
 +255 652397343


No comments: